Saturday, 24 January 2015

ARSENAL NJIA NYEUPEEE KWA PAULISTA


Na Ramadhani Ngoda.
Bosi wa Arsenal, Arsene Wenger yuko katika harakati za kunasa saini ya beki wa kati kwa ajili ya kuimarisha safu yake ya ulinzi mwezi huu.
Na jicho lake limelenga kwa mlinzi wa kibrazil, Gabriel Paulista kutoka Vilareal ya Hispania.
Gabriel Paulista

  Ni kama mpango wa Arsenal kumsajili Paulista mwezi huu wa januari umepata nguvu baada ya beki huyo mwenye thamani ya paundi milioni 15 kuachwa katika kikosi cha Villarrealkinachoivaa Levante wikiendi hii.
 Villarreal walitangaza kikosi cha wachezaji 18 kinachochuana na Levante uwanja wa El Madrigal na waliorodhesha wachezaji watakaokosa mechi kwasababu ya majeruhi na kutumikia adhabu.

Japokuwa kuachwa kwa jina la Paulista, klabu haijatoa sababu katika tangazo lake, lakini  inaripotiwa kuwa nyota huyo yuko njiani kutimka. Na Emirates kunaweza kuwa fikizio lake.
Lakini  Arsenal wanaweza kukumbana na kikwazo kingine  kutoka kwa shirikisho la soka nchini Uingereza (FA) cha kupata kibali cha kazi kwa beki huyo raia wa Kibrazil.
Arsene Wenger- kocha wa Arsenal

Na Arsene Wenger amelilalamikia suala la utaratibu na kanuni za utoaji vibali kwa wachezaji wageni nchini Uingereza.

No comments:

Post a Comment